BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Thursday, July 29, 2010

WALAKA KWA WASANII WA MUZIKI KABLA YA UCHAGUZI 2010

Kuelekea uchaguzi mkuu mwezi october mwaka 2010,huu ni walaka wangu kwa wasanii wote wa muziki wa kibongo!. Najua kuna miaka mingi sana ya kuukomboa huu mziki wetu lakini wazungu wanasema "One step at a time"...na muda ndio huuu..........!!!! 

 MTOTO WA VITOTO

Miaka kibaao sasa wasanii mmekuwa mkilalamika juu ya kudhulumiwa haki zenu kwa kuibiwa kazi zenu na kulipwa malipo madogo ya album zenu kiwango kisichokidhi mahitaji yenu,hilo ni sawa kabisaaa!!

LAKINI je!! mmejipanga vp kumaliza hili tatizo lenu? kila kukicha viongozi wanawa-ahidi kwa mdomo kuwa watamaliza tatizo lenu bila utekelezaji wa vitendo kitu ambacho mimi nakiona kama ni kiini macho na nyinyi wenyewe mnakifahamu....







Viongozi hawa hawa ambao wanakataa kwa "makusudi" kusimamia maslahi yenu ndio hao hao wanaokuwa wa kwanza kuwachukua nyinyi wakati wa uchaguzi ili muwasaidie kuwapigia kampeni kwa kutoa burudani pindi wanapokuwa kwenye mikutano yao,,,,

Sasa inakuwaje mnatumika kirahisi namna hii? wakati kwenye interview zenu wengi wenu mnajinadi kuwa nyinyi ni wanaharakati na sasa mnafanya mageuzi ya huu mziki wenu,vp mageuzi ndio haya? Mnapotumiwa kwenye kampeni mnacheka cheka kwa furaha pale mnapopewa laki kadhaa au vimilioni kama shukrani ya "kinafki" kutoka kwa hao watu waliowatumia!!!! Na baada ya kumaliza kampeni zao hao hao wakiwa madarakani wanawasahau na kujifanya hawawakumbuki tena hadi wakati mwingine wa uchaguzi.....(huu ni utumwa wa kifikra) najua mtasema mnaangalia pesa na ndio mana mnawafanyia kazi yao na sio kitu kingine!!! Sawa sikatai huenda ni kweli pesa ndio mnayofuata,,, sasa je? nyie wasanii wa kiume ikitokea wamama wakiwapa pesa za kutosha na kuwataka mkatumbuize kwenye "kitchen party" yao mtaenda kudhalilishwa sababu ya pesa au mtakataa?

Sidhani kama ntapata dhambi nikisema kuwa kitendo cha wasanii kutumiwa kwa muda na hawa watu mi nakifananisha na binti wa kike ambae bwana wake huwa anajifanya kumjali na kumfuata pale anapotaka penzi lake tu!! na akishamaliza shida zake anaondoka na kumuacha binti huyo akiteseka na hali ngumu ya maisha bila ya msaada wowote na hurudi tena pale anapokuwa na shida hiyo!!

Enyi wasanii kwanini mnajipa thamani ndogo kiasi hicho???
Huu ndio wakati wenu wasanii kuonesha mapinduzi yenu na misimamo yenu na zile harakati ambazo kila kukicha mmekuwa mkizitaja kwenye nyimbo zenu na interview zenu,,,yawapasa kudai maslahi yenu kwanza kuliko kutumika kuhangaikia maslahi ya watu wengine....

Sitoona ajabu nikiwaona wasanii wale wale wanaokuwa wa kwanza siku zote kudai haki zao wakitumika kwenye kampeni mwezi october na kisha baada ya uchaguzi mwakani wasanii hao hao tutawaskia tena wakilalamika kutokumbukwa na viongozi husika!!!

"CALCULATE THE RISK,BEFORE YOU JUMP"
                                                               By Mtoto wa vitoto..
(Ze' son of babiez)
2010...

Wednesday, July 28, 2010

fiesta mwaka huu twajipangusaje????

vituko mbali mbali vinavyoendelea kujili katika fiesta mikoani.

sijui ni mapumziko au hebu ngoja tuone hapo chini

mmmh kumbe ndo hv duh jipanguse na tairi
on the move to hotel
hapa jee!!
haya tumeona kote hiko na hii ni show pale kati A city arachuga wat abt bongo yetu ni lini wazeiya??!!

Show ya kwanza ya Rap iliyopangwa kufanyika katika mji mdogo wa Branson, Missouri nchini marekani imeingia kwenye utata na maofisa wa mji huo. promota wa Concert hiyo Paul Dunn alitaka show hiyo ipigwe katika sehemu ya Parking ya ukumbi wa The Grand Palace kutokana na ukumbi huo kufanyiwa matengenezo kwa ndani. Parking hiyo inauwezo wa kuingiza watu 6000 wakati ndani ya ukumbi huo kunaweza kuingia watu 4000.

kwa mijibu wa chanzo chetu cha habari kinasema kuwa mkurugenzi wa mipango miji wa Missouri amechomoa ombi la waandaaji wa Concert hiyo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo makelele, Parking, na udhibiti wa watu watakao kuwepo siku hiyo. Mkurugenzi huyo pia amelalamika kuwa waandaaji wa Concert hiyo wanaendelea kupromote kuwa mtu mzima Nelly atapanda katika stage tarehe 21 August na pia tayari wameanza kuuza ticket za onyesho, huku wakitambua bado makubaliano hayajafikiwa.

Waandaaji wa Concert wamesema wanashangaa kuulizwa maombi mapya wakati tangu awali walishapeleka maombi, jamaa wanampango wa kukata rufaa kwa board ya jiji. Rufaa ya waandaji itaambatana na vielelezo vya mpangilio wa ulinzi utakavyo kuwa siku hiyo, pamoja na Documents zenye Signature za majirani wa eneo husika, wakithibitisha kuwa wao majirani wamebariki Concert hiyo kufanyika Branson.

inasemekana concert hiyo itaingizia mji wa Branson mapato ya dola za kimarekani laki tano.
  
Inawezekana uongozi wa mji huo unabana mchongo kwa sababu za kihistoria kwani mji wa Branson ni mji flani uliopooza na pia kipindi cha nyuma asilimia kubwa ya wakazi wake walikuwa ni wapenzi wa Country Music, hata wakongwe wa mziki wa Country nchini marekani kama Kenny Rogers, Wyne Newton na Pat Boone wanaishi Branson.( Yaani pamoja na muziki wa Hip Hop kuanza miaka mingi nchini marekani lakini wakazi wa mji wa Branson hawajawahi kushuhudia mwanamuziki wa Hip Hop akikanyaga jukwaa lao hata siku moja) Aiseeeee.... Dar es salaam wamekuja Rapper wangapi kutoka nchini marekani? Jiulize?

hata sisi tunawashinda Branson, na huku ni Thousands of miles....

Kwa mujibu wa waandaaji wa Concert tayari mashabiki elfu tatu wamekwisha nunua Ticket ili Kumshuhudia Mtu mzima Nelly na kundi lake la Saint Lunatics wakishusha swager za Hip Hop kwa mara ya kwanza ndani ya mji wa Branson.

NGOMA JIPYA LA TEMBA NA CHEGGE "FUNGENI MKANDA"

Chegge na Temba wanatarajia kutoa track mpya itakayoitwa "Vijana Fungeni
Mkanda"
Chanzo changu cha habari kimeinyaka hii huku jamaa wakiwaambia mashabiki wao wakae tayari
kupokea song lao hili
                                 kwani litakua ni moto wa kuotea mbali ukiachia ile ya
                                                                   'Mkono Mmoja'

             Jamaa kwa Sasa wako kwenye tour ya fiesta wakikamua mwanzo mwisho na
                   wamewaambia mashabiki wao kukaa tayari kwani album yao pia iko sokoni karibuni.


Msanii nyota wa filamu hapa nchini Daudi Michael amekamilisha utayarishaji wa filamu zake na hivi sasa zimeanza kuingia sokoni moja kati ya filamu ambazo zimeingia sokoni ni Fake pregnant na moja ambayo haaijatoka kwa sasa Aunt suzzy.ambazo ametayarisha hivi karibuni.
Amesema kuwa filamu hizo ni bomba na zinazungumzia maisha halisi ya kitanzania.

 DVD cover ya filamu ya Fake Pregnant part one

DVD cover ya filamu ya Fake Pregnant part two.
Pia amesema kuwa wasanii nyota walioshiliki katika filamu hizo ni kama Esther,sarah sudi, sudi,santana na wengine nyota kibao na wasanii vichwa wachanga.

DVD cover ya filamu ya Aunt Suzzy part one.
DVD cover ya filamu ya Aunt Suzzy part two.
Zaidi msanii huyu wa filamu hapa nchini ameshatoa filamu kadha wa kadha kutoka katika kampuni yake ya D production kama vile Where is love, Upside Down, Remember na nyingine kibao.na amewahi kushiriki katika movies nyingine kama money desire,kisisina and many more.
Hivyo amewaomba watanzania wamuunge mkono katika kazi yake kwa kununua nakala halisi ili tasnia nzima ya filamu iweze kusonga mbele na ameahidi utakapo nunua filamu hizi hutajutia maamuzi yako. 
Wabongo tumuunge mkono mbongoo mwenzetu tuachane na mambo ya kale ya tamthilia za kiphillipino eti jamani.........!!