BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Friday, October 1, 2010

"The Sporah Show " mbadala wa show ya oprah hapa bongo.


Tumezoea kuwaona watangazaji na waendesha vipindi vya televisheni maarufu kama vile Oprah Winfrey na kipindi chake Oprah Winfrey Show na Tyra Banks na kipindi chake The Tyra Banks Show wote hawa wakiwa ni wanawake wa Kiafrika wenye asili ya Marekani waliofanikiwa na kujizolea umaarufu kutokana na vipindi vyao hivyo.

Pamoja na kuwa ni Wamarekani weusi, lakini bado tukiwa kama Watanzania hatuwezi kujitapa ama kujivunia sana pamoja kwamba kwa asili wana damu ya Kiafrika.
Sporah akiwa na alikiba pamoja na Mims.

Lakini sasa huenda umefika wakati wetu nasi kujivunia watu wetu, watangazaji wetu, Watanzania wenzetu ambao wameamua kuvunja ukuta na kujitosa katika uendeshaji wa vipindi ama maonesho ya televisheni kama ilivyo kwa Oprah na Tyra.

Tuna kila sababu sasa kama watanzania kujivunia kwa sababu tumepata Mtanzania mwenzetu ambaye ameamua kuendesha kipindi cha mazungumzo katika televisheni, na huyu si mwingine bali ni Irene Sporah Njau ambaye ameanzisha Kipindi cha Majadiliano cha Kiafrika kinachojulikana kama The Sporah Show akiwa nchini Uingereza.
Irene Sporah Njau.
 
Kama hiyo haitoshi, binti huyo kutoka Tanzania ambaye hujulikana zaidi kwa jina la Sporah kuanzia Juni 11 The Sporah Show itakuwa ikioneshwa hapa nyumbani kupitia kituo kimojawapo cha televisheni nchini katika siku za Ijumaa na Jumamosi

"Kwa kweli TV Show ilikuwa ni ndoto yangu, ila nilipofika Uingereza na kuona jinsi ambavyo nchi za wenzetu zina mifumo tofauti ya kuelimisha jamii, nilijikuta vikinipa motisha zaidi ya kutaka kutimiza ndoto yangu ndipo nilipopata wazo la kuanzisha kipindi cha The Sporah Show" asema Irene Sporah Njau.

Usiku wa Kanga kufanyika leo usiku



Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Chiku Galawa, anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika ‘Usiku wa Kanga za Kale’ utakaofanyika Oktoba mosi kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam
 .

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Fabak Fashion, Asia Idarous, tamasha hilo litashirikisha wabunifu wa mavazi na wadau mbalimbali, wakiwemo kina mama na kina baba watakaopanda jukwaani kuonyesha mavazi ya kanga na vionjo.

Idarous alisema tamasha hilo litasindikizwa na burudani kutoka kundi la Jahazi Modern Taarab, waimbaji nyota Khadija Kopa, Rukia Ramadhani, Sabah Salum Muchacho na Baby Madaha.

Aidha, Idarous alitaja viingilio katika usiku huo kuwa ni shilingi 20,000 kwa viti maalumu ‘VIP’ na shilingi 10,000 kwa viti vya kawaida, ambako tiketi zinapatikana Fabak Fashions.

usiku huo wa kanga wataoonesha mavazi ni macelebrity wa bongo wakiwemo waigizaji wa filamu, wadau wa mitindo na watu kadhaa wanaofahamikatika sekta tofauti tofauti

Sunday, September 26, 2010

'East African Bash' yawakutanisha AY Amani na Ngoni ndani ya Da’ West.

Wasanii Ambwene Yesaya `AY`’ kutoka Tanzania, Ngoni kutoka Uganda na Amani wa Kenya, wanatarajiwa kuonyeshana kazi jijini Dar es Salaam kesho katika tamasha maalum la muziki lililopewa jina la 'East African Bash' na kushirikisha nyota wa nchi hizo wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashairiki.



AY na wakali wenzake hao, watachuana kwenye ukumbi wa Da’ West uliopo Tabata na baada ya hapo, watachuana tena katika onyesho la pamoja litakalofanyika siku moja baadaye kwenye eneo la ufukwe wa Mbalamwezi jijini Dar.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, AY ambaye ni mmoja wa washiriki, alisema amejipanga kuwawakilisha vyema Watanzania kwa kuonyesha kiwango cha juu na kuwaduwaza wanamuziki kutoka Kenya na Uganda.

"Najua hili ni tamasha kubwa na mimi ndiye niliyebahatika kuwa mwakilishi pekee wa Tanzania… kwa sababu hiyo, nataka kufanya kweli ili kuwakilisha vyema," alisema AY.

Kwa upande wake mratibu wa tamasha hilo, Dennis Busulwa, alisema kuwa lengo kubwa la tamasha hilo ni kuendeleza umoja wa wanamuziki wa nchi za Afrika Mashariki.