BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Saturday, August 13, 2011

PRUDENCE KIBAYA:Tunda jipya la Tusker Project Fame 4

Alianza kuimba kabla ya kushiriki katika mashindano ya Tusker Project Fame Season 4, Prudence Kibaya ni mmoja wa wasanii chipukizi ambao maisha yao ya kimuziki yanatarajiwa kuwa bora zaidi siku za usoni.
Baada ya kushiriki kwenye mashindano hayo ya TPF4, mwanamuziki huyo chipukizi alitoa kibao kiitwacho 'Nataka Cheza' akimshirikisha mwanamuziki maarufu wa mjini Mombasa aitwaye Labalaa.
Licha ya kuwa alikuwa anapenda kuimba, Prudence alijitosa katika dunia ya muziki miaka miwili iliyopita akiwasaidia wasanii wengine katika studio za kurekodia muziki.


Katika kipindi hicho, Prudence pia alifanya 'kolabo' na msanii wa Mombasa, Husler J katika wimbo uitwayo 'Minyororo ya Haki'.
Kwa sasa wakati kibao chake kipya kiitwacho 'Shuka' kinavuma nchini, Prudence anakubali kuwa fursa aliyoipata ndani ya TPF4 ilimpatia mafunzo mengi kuhusu muziki.
Akiwa mwanafuzi wa taaluma ya habari katika Chuo Kikuu cha Mombasa Polytechnic, Prudence anasema kuwa anatayarisha albamu ambayo ananuia kuizindua mwishoni mwa mwaka.
Ingawa alizindua kibao 'Shuka', mwanamuziki huyo chipukizi anasema kuwa yuko na vibao vingine ambavyo kwa sasa viko studioni. Kwa sasa, anasema, tayari ana mkataba wa kurekodi nyimbo tano na Grandpa Records huku akiongeza kwamba anajiandaa kufanya 'kolabo' na mwanamuziki mwingine maarufu Afrika Mashariki, Nyota Ndogo.

Prudence anasema kuwa anaweza kufanya shoo za muziki katika sehemu yeyote nchini wakati wowote atakapohitajika, lakini akaongeza kwamba anafarijika kutokana na maoni mengi anayoyapata kutoka kwa mashabiki wake kupitia mtandao wa internet.
Akaongeza kwamba ananuia kuanzisha bendi yake mwenyewe ya muziki ambayo itawahusisha wasichana peke yao na kuwa na matumaini kwamba huenda akaweka rekodi ya kuwa na kikundi cha wasichana pekee kitakachokuwa maarufu na kutoa burudani.











Thursday, August 11, 2011

REDDS YATOA ZWAI KWA WAREMBO MISS TANZANIA.


Meneja wa kinywajicha redd’s, Victoria Kimaro akimkabidhi mshiriki namba 26 kutoka kinondoni Husna maulid vifaa maalumu vitakavyotumiwa na warembo wa Miss Vodacom Tanzania 2011 wakati wa mazoezi jijini Dar es Salaam. 
 Baadhi ya Washiriki wa kinyanganyiro cha kumsaka Miss  Tanzania 2011 wakianagalia vifaa walivyokabidhiwa jana na kutoka kinywaji cha Redd’s kwaajili ya kuwasaidia wakati wa mazoezi jijini Dar es Salaam.

 Baadhi ya Washiriki wa kinyanganyiro cha kumsaka Miss  Tanzania 2011 wakianagalia vifaa walivyokabidhiwa jana na kutoka kinywaji cha Redd’s kwaajili ya kuwasaidia wakati wa mazoezi jijini Dar es Salaam.

Meneja wa kinywajicha redd’s, Victoria Kimaro akimkabidhi Layla Juma jana vifaa maalumu vitakavyotumiwa na warembo wa Miss Vodacom Tanzania 2011 wakati wa mazoezi jijini Dar es Salaam.




Monday, August 8, 2011

VIMWANA 30 WA VODACOM MISS TANZANIA 2011 WAINGIA KAMBINI LEO KATIKA VODACOM HOUSE



Mkuu wa Udhamini wa Vodacom Tanzania, George Rwehumbiza (kulia) akiwa na Mkurugenzi wa Lino International Agency, Hashim Lundenga waandaji wa Vodacom Miss Tanzania wakizungumza na warembo wanaowania taji la Miss Tanzania 2011, baada ya kuwasili katika kambi yao iliyopo Hotel ya Giraffe Ocean View Mbezi Beach jijini Dar es Salaam jana.


Waremmbo wanaowania taji la Vodacom Miss Tanzania 2011, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kuwasili katika kambi yao iliyopo Hotel ya Giraffe Ocean View Mbezi Beach jijini Dar es Salaam jana.


Vodacom Miss Tanzania 2010, Genevieve Mpangala (katikati mwenye miwani) akigonganisha glasi ishara ya kuwakaribisha warembo wanaowania taji la Miss Tanzania 2011 baada ya kuwasili katika kambi yao iliyopo Hotel ya Giraffe Ocean View Mbezi Beach jijini Dar es Salaam jana.

Na Mwandishi Wetu

JUMLA ya warembo 30 kutoka kanda tofauti nchini leo (jana) wameanza rasmi kambi ya Vodacom Miss Tanzania 2011 yaliyopangwa kufanyika Septemba 10 kwenye ukumbi wa Mlimani City kwa mfumo tofauti na ule uliozoeleka miaka ya nyuma ambapo warembo walikuwa wakikaa kambini katika Hotel ya Giraffe iliyopo jijini Dar es Salaam.

Vodacom Tanzania ambao ndio wadhamamini wakuu wa shindano la Vodacom Miss Tanzania kwa miaka kadhaa mfululizo safari hii wamebadilisha kabisa muundo wa awali na hivyo walimbwende hao watakaa ndani ya jumba maalum lililopewa jina ‘Vodacom House’.

Mkuu wa Udhamini wa kampuni hiyo George Rwehumbiza amesema jijini Dar es Salaam kuwa lengo la kufikiwa kwa mabadiliko hayo ni kulifanya shindano hilo liwe na muonekano tofauti kama ilivyo kwa Vodacom ambayo imebadili muonekano wake na kasi ya utoaji huduma.

“Safari hii warembo 30 wanaoshiriki shindano hili la Vodacom Miss Tanzania wataishi kwenye jumba maalum ‘Vodacom House’ na humo watafundishwa vitu mbalimbali ikiwemo jinsi ya kukabiliana na vishawishi hususan katika masuala ya kimapenzi,” alisema Rwehumbiza.

Akitaja malengo mengine ya kuwaweka washiriki hao ndani ya jumba hilo Mkuu huyo wa udhamini alisema kampuni yake kwa sasa inatoa huduma kwa teknolojia yenye kasi zaidi hivyo warembo hawana budi kuendana nayo kwa kufundishwa aina ya kula, kuondoa ulimbukeni mara wanapopata umaarufu.

Mabadiliko haya yatalifanya shindano hili kuwa bora na linaloenda na wakati kama zilivyo huduma zetu yaliyotokana na mabadiliko ya nembo yetu. Wakiwa ndani ya jumba warembo watakaa kwa wiki tatu wakijifunza masuala ya kijamii, alisema Rwehumbiza.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Lino Agency waandaaji wa shindano hilo Hashim Lundenga amesema kwa mwaka huu wanataka warembo wenye sifa ikiwemo elimu, muonekano na tabia nzuri ili mshindi atakayepatikana aweze kutuwakilisha vema katika medani za kimataifa.

“Sisi hatuangalii mshiriki ametoka wapi iwe kijijini au mjini, tunachozingatia ni mrembo kukidhi viwango vya shindano ikiwemo sifa tunazozitaka ili mwisho wa siku kila mtu ajivunie mafanikio aliyoyapata akiwa ndani ya jumba la Vodacom House na atumie kigezo hicho kufanikiwa kimaisha,” alisema Lundenga.

Lundenga alisema kuwa mfumo wa mashindano ya mwaka huu, umebadilika ambapo jumla ya warembo 15 wataingia hatua ya nusu fainali baadala ya 10 kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.

Alisema kuwa kati ya warembo hao 10, watano watapatikana katika mashindano maalum wakiwa katika Vodacom House. Kwa mujibu wa Lundenga, kutakuwa na mashindano ya Top Model ambayo yatafanyika leo na baadaye kufuatiwa na mashindano ya Vipaji (Talent), Mrembo bora wa muonekano katika picha (Miss Photogenic), Mrembo bora wa michezo (Top Sports Woman) na mrembo atakayeonyesha ushirikiano mkubwa na uchangamfu katika kambi, Miss Personality.

Ili kuishirikisha jamii, maisha ya washiriki hao wa Vodacom Miss Tanzania 2011 ndani ya Vodacom House yatakuwa yakioneshwa moja kwa moja ‘Live’ na vituo vya Startv pamoja na Clouds TV ili kutoa nafasi kwa watazamaji kumpigia kura mrembo anayefaa kuvikwa taji hilo na kumrithi Genevieve Mpangala mshindi anayemaliza muda wake.

Picha Na John Bukuku - Full Shangwe Blogu

Sunday, August 7, 2011

CHUO CHA TSJ CHANG'ARA KWENYE MASHINDANO YA UTANGAZAJI..


Mkuu wa Chuo Cha TSJ Bi Setumbi

CHUO cha Uandishi wa habari cha Time School of Journalism (TSJ) kieibuka mshindi wa kwanza katika mashindano ya kitaaluma yaliyoshirikisha vyuo vinne vya taaluma hiyo jijini Dar es Salaam.

Vyuo ambavyo vilishiriki katika mashindano hayo ni Time School of Journalism (TSJ), Royal College of Tenzania (RCT), Dar es Salaam School of Journalism (DSJ), na Dar es Salaam City College (DASICO).

Katika mashindano hayo yaliyofanyikamwisho wa wiki iliyopita katika chuo cha uandishi wa habari cha Royal (RCT), TSJ waliwazidi washindani wake kwa kupata alama za jula 887, wakifuatiwa kwa mbali na RCT waliopata alama 880.

Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Chuo cha Dar es Salaam City College (DASICO) na DSJ wakiwa ni washindi wa mwisho katika mashindano hayo.

Vipengele vilivyoshindanishwa katika mashindano hayo ya utangazaji ni mwanzo wa habari, kusoma habari, kuandaa vipindi makini, vipindi vya burudani na vya michezo.

Akieleza ushindi huo, Waziri wa Habari serikali ya wanafunzi wa TSJ (TISJOSO), Jestina Joseph, alisema uamuzi wa kuwashindanisha wanafunzi kitaaluma ni mzuri na una lengo la kuwajenga ki elimu zaidi.

“Tunaamini mashindano haya yatakuwa endelevu ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kushindanishwa kujenga uwezo na ubunifu katika taaluma hii ya uandishi wa habari na utangazaji,” alisema Jestina.

Naye Waziri Mkuu wa serikali ya wanafunzi ya TISJOSO, Bwana Hamad Amour alieleza kuwa chuo chao kuliona ni vyema kushiriki katika mashindano haya ili kujenga uelewa wa taaluma hii na kuona jinsi vyuo vingine wanavyofundishwa katika taaluma hii.

Wakati huo huo Amour aliongeza kuwa serikali yake iko katika hatua za mwisho za maandalizi ya sherehe ya kuwakaribisha mwaka wa kwanza inayotarajiwa kufanyika tarehe 3 September katika viwanja vya Jangwani Sea Breeze na amesema kuwa sherehe hiyo itawakutanisha tena wanachuo wenzao kutoka vyuo vingine hivyo ambavyo navyo vinatoa taaluma ya habari.

“Katika sherehe hiyo ya kuwakaribisha mwaka wa kwanza kutakuwa na michezo mbali mbali ambayo itawajenga wanafunzi na kuwaandaa wageni walioingia chuoni hapa kwa ajili ya kupata taaluma ya habari,” alieleza Amour.

Aliongeza kuwa mbali na kuburudika kwa michezo mbali mbali katika sherehe hiyo ni wakati wa kukutana pia na waandishi pamoja na wahariri wa habari kutoka vyombo mbali mbali vya habari hapa Tanzania kuzungumza nao ili nao watupatie elimu itakayo tuandaaa kuelekea kazini.

“Tunatarajia kualika wadau mbali mbali wa habari ambao tutajumuika nao pamoja katika sherehe hii ili kubadilishana nao mawazo na kujifunza mengi kutoka kwao na pia tutakuwa na mgeni rasmi kutoka serikalini ambaye tutawajulisha badae ni nani atakaye kuja kwani bado tuko katika mawasiliano nae,” aliongeza.