BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Friday, December 17, 2010

MSHINDI WA BONGO STAR SEARCH 4 NI MARIAM MOHAMED


MSHIRIKI wa shindano la kusaka vipaji vya uimbaji la Bongo Star Search,MIRIAM MOHAMED mwenye namba ya ushiriki BSS 17 Ameibuka mshindi kwa kujinyakulia kiasi cha shilingi milioni 30 kutoka kwa wadhamini wakuu wa Shindano hilo ambao ni TBL kupitia kinywaji cha Kilimanjaro Premium Lager.
 
Mariam Mohamed.


Mshindi wa pili wa shindano hilo ni... James Martin BSS 14 ....ambaye amejinyakulia kitita cha shilingi milioni kumi kutoka kwa wadhamini wenza wa shindano hilo ambao ni Airtel.
 
 James Martin.

Na mshindi wa tatu ni... joseph Payne BSS 07....ambaye amejinyakulia kiasi cha shilingi milioni tano 
joseph Payne.
Wakifuatiwa na Bella Kombo. ambaye ni mshindi wa nne na Waziri Salum ambaye ni mshiriki namba BSS 11 ambaye ni mshindi wa tano wa shindano hilo
Bella Kombo.
 
Waziri Salum. 

Wednesday, December 15, 2010

MARLAW,CHEGE KUTUMBUIZA BSS IJUMAA.



NYOTA kadhaa wa muziki wa kizazi kipya wakiwemo Marlaw, Diamond, Chege na Mh Temba watatumbuiza katika fainali ya kumsaka kinara wa shindano la ‘Kilimanjaro Bongo Star Search 2010’ kwenye ukumbi wa Mlimani city jijini Dar Es Salaam ijumaa.

 Ritha Paulsen na Meneja wa TBL.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam jana, mkurugrnzi  wa kampuni ya Benchmark Production inayoandaa shindano hilo, Ritha Paulsen, aliwataja nyota wengine watakao tumbuiza siku hiyo kuwa ni Mwasiti, Joh makini, Imani na Cindy kutoka nchini Uganda.
Alisema kuwa fainali hizo zitaoneshwa na moja kwa moja na kituo cha televisheni cha ITV kuanzia saa 1:00 usiku na maandalizi yote yamekamilika.
Nyota watano walioingia fainali na kuwania zawadi ya Kwanza ya  kitita cha Sh. Milioni 30 ni Bella Kombo mwenye namba BSS 02, joseph Payne BSS 07, Mariam Mohamed BSS 17, James Martin BSS 14 na Waziri Salum ambaye ni mshiriki namba BSS 11.
 Washiriki wakionesha zawadi ya mshindi wa kwanza.

Mshindi wa pili atapata Sh. Milioni 10 huku watatu akitarajiwa kuzoa Sh. Milioni tano.
Ritha alisema zawadi ya kwanza imetolewa na wadhamini wakuu wa shindano hilo, kampuni ya bia ya TBL kupitia bia yake ya Kilimanjaro, wakati zawadi ya mshindi wa pili imetolewa na kampuni ya huduma ya simu za mkononi ya Airtel.
 Tano bora ya BSS 2010.

Meneja wa bia ya Kilimanjaro, George kavishe, alisema kuwa kampuni yake imeungana na Benchmark katika shindano hilo kwa nia ya kuibua vipaji vya muziki wa Tanzania.
Bella Kombo na joseph Payne  

Monday, December 13, 2010

FAINALI YA BSS 2010 KUFANYIKA IJUMAA.


HATIMAYE washiriki watano wameingia fainali za shindano la Bongo star search na watachuana kumtafuta mshindi katika fainali itakayofanyika Ijumaa kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar Es Salaam.
Washiriki hao wameingia katika hatua hiyo baada ya washiriki wenzao watatu kutangazwa kuaga shindano hilo jana wakati walipofanya 'shoo' kwenye ukumbi wa Water front na kurushwa na kitua cha televisheni cha ITV.
Shoo hiyo ilipambwa na wasanii nyota kadhaa wakiwemo Banana Zoro, Mwasiti, Tundaman, Maunda zoro, Amini, Barnaba, Marlaw na Patricia hilal, amabo waliimba pamoja na washiriki wa BSS.

Washiriki watano walioingia katika fainali hiyo baada ya kupigiwa kura nyingi kutoka kwa wananchi ni Waziri salum, Bella Kombo, James Martin, Joseph Payne na Mariam Mohamed.
Washiriki watatu walioaga michuano baada ya kupata kura chache ni Christabella nzowa, Haji Ramadhani na Chiby Dayo.
Mshindi wa BSS mwaka huu atajinyakulia zawadi ya shilingi milioni 30.

DK REMMY ONGALA AFARIKI DUNIA.


Habari za kusikitisha zilizofikia leo asubuhi hii ni kwamba msanii maarufu hapa Tanzania mwenye asili ya kiZaire, Dr. Remmy Ongala, amefariki dunia.
Inasadikika kwamba Ongala alipelekwa hospitali kuu ya Muhimbili jijini Dar es salaam baada ya kuzidiwa usiku wa Jumapili. Alitangazwa marehemu mapema Jumatatu baada ya hali yake kuzidi kuwa mbaya na madaktari kushindwa kumsaidia.
Remmy Ongala atakumbukwa zaidi kwa ustadi wake kwa kupiga guitar na uimbaji wake ambao uliweza kuzivuta hisia za wengi kwa miaka 30 aliyokuwa akishughulika na muziki.
Tunaiombea familia ya Dr. Ongala faraja na Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Fally Ipupa na 2Face Vinara Tuzo za Mama MTV.


Wasanii Fally Ipupa kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo pamoja na 2face Idibia wa Nigeria Jana usiku wameibuka vinara wa tuzo za MaMa’z kwa mwaka 2010 baada ya kujinyakulia jumla ya tuzo mbili kila mmoja.
Wasanii hao walikuwa wanawania tuzo zaidi ya tatu katika vipengele tofauti na baadaye kujinyakulia tuzo za Video bora. Msanii bora wa Francophone ilienda kwa Fally Ipupa wakati  2Face akibeba Msanii wa mwaka na msanii bora wa kiume.

Sherehe hizo za kuwatuza wasanii wa kiafrika zilianza mida ya saa moja jioni ambapo wasanii mbali mbali pamoja na wageni waalikwa waliwasili katika eneo la Red Carpet kabla ya kupiga picha na kujipatia vinywaji vilivyokuwa tayari kabisa kwa ajili ya wageni hao.
Msanii wa Tanzania Diamond aliondoka mikono mitupu licha ya kupata nafasi ya kuimba pamoja na P-Unit na Teargas katika jukwaa moja.

Aidha sherehe hiyo zilianza rasmi majira ya saa tatu na nusu ambako msanii kutoka Marekani Rick Ross alikuwa wa kwanza kupanda jukwaani na kuamsha nderemo, vifijo na kelele za kutosha ukumbi mzima kabla ya kutoa fursa kwa tuzo ya kwanza kabisa kutolewa ambayo ilikuwa video bora iliyokwenda kwa Fally Ipupa.
Wasanii wengine waliopiga shoo ni pamoja na Moze Radio na Weasle, Jozi, Big Nuz, Sasha, Cabo Snoop, Barbara Kanam, Fally Ipupa, J Martins, 2 Face, Wande Coal, T-Pain, Mo Cheddah  na Eve.

Baadhi ya watu maarufu waliokuwemo katika tuzo hizo ni pamoja na mchezaji wa mpira J J Okocha, Tatiana Durao, Munya na mmiliki wa kituo hicho cha televisheni cha MTV, Bw. Tedd Turner.

Sherehe hizo za kutuza wasanii wa kiafrika za MAMAs zimeletwa kwenu kwa udhamini wa Airtel, Master Card, Halmashauri ya Jiji la Lagos pamoja na hoteli ya nyota tano Eko Suites ambako ukumbi wake wa Eko Center ulitumika.