BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Saturday, July 3, 2010


COMING SOON 

KUPITIA KING'AMUZI CHA STARTIMES NI SIBUKA TV KATIKA MAENENEO YA MWANZA , DAR , ARUSHA NA DODOMA UTAPATA NAFASI YA KUBURUDIKA NA KUHABARIKA NA KITUO HIKI BORA CHA TELEVISHENI KITAKACHOKUJIA HIVI KARIBUNI

104.9 fm, 97.0fm, 94.0 fm hii ni sibuka fm! PIA KUPITIA KING'MUZI COMING SOON NI SIBUKA TV

Kwa taarifa na burudani ni station hii tuu ndo yaweza kukupatia kile unachokihitaji katika nyaanja zote za burudani na habari.

 headphone
Kutana na member wa sibuka fm na fahamu vipindi vyao kila siku za wiki.

 MARK EVANC katika pambazuko lafrika mashariki


 KAMAL ABDUL katika kipind cha 180 power


moja ya mic ya studio 

JUMA BAKARI(JB)ndani ya pepeta Afrika na KAMAL ABDUL




COMING SOON KUPITIA KING'AMUZI CHA STARTIMES NI SIBUKA TV KATIKA MAENENEO YA MWANZA , DAR , ARUSHA NA DODOMA UTAPATA NAFASI YA KUBURUDIKA NA KUHABARIKA NA KITUO HIKI BORA CHA TELEVISHENI KITAKACHOKUJIA HIVI KARIBUNI




SIKILIZA BAABKUBWA SAA 10:00 USIKU MPAKA SAA 01:00 USIKU KUPITIA SIBUKA FM



NI SHOW KALI NA YA KIJANJA INAYOKUPA NAFASI KUSIKILIZA NGOMA KALI ZA MTONI, BONGO FLAVA, UGANDA KENYA NA NYINGINE NYINGI.



Kutana na frank Aman Mawenya aka Tha Zealot katika show hii kupitia sibuka fm 94.0 kwa Pwani na Dar, 97.0 kwa Maswa na 104.9 kwa Shinyanga na kupitia Satelite kwa Audio Four katika upande wa kulia(right) kwenye TBC1 Television




BAAAAAAAAABKUBWAAAAAAAA!

TUZO ZA BET SASA HIVI KATIKA BLACK ENTERTAINMENT TELEVISON




Tuzo za wasanii wa muziki wa Hiphop na RnB wenye asili ya kiafrika zilizofanyika tarehe 27.06.2010 zinaonyeshwa live sasa hivi katika television ya BET.



 Nakusihi mdau wangu utazame kupitia katika vingamuzi vya STARTIMES ambavyo unapata nafasi ya kuona channel hiyo kwa hapa TZ.


Friday, July 2, 2010

SIKILIZA SIBUKA FM KWA PWANI, DAR, MASWA, NA SHINYANGA katika fm PIA SATELITE DUNIA NZIMA KUPITIA TBC 1 katika audio 4 right

                                          kamal abdul

VIPINDI:
1.Pambazuko la Africa ya Mashariki.with Stivin Mumbi
2.Safari mseto with Monica
3.180 power with Dj Mark and kamal abdul
4. (Taarifa Ya Habari)pepeta Africa with JB.
5. Sports with Mark Evanc
6.Crossfire with Christina Mwakangare
7.Maisha Changamoto with Kamal Abdul
8.Mkesha wa kazi with Frank Aman(tha Zealot).
9.Amka na Sibuka fm with Frank Aman and Erick




SIKILIZA KUPITIA FM 94.0 DSM NA PWANI,97.0 MASWA, 104.9 SHINYANGA na KUPITIA SATELITE KWA TBC 1 TELEVISION.

TUZO ZA BET FUNIKA BOVU NIKKI MINAJ AUWAA

Best Female Hip Hop Artist: Nicki Minaj, Best New Artist: Nicki Minaj,
Best Male Hip Hop Artist: Drake, Best Group: Young Money


didy na busta rhymes wakiperfom juu ya stage ya BET siku ya tarehe 27 yaahi jana


Best Male R&B Artist: Trey Songz


Best Female R&B Artist: Alicia Keys, Best Collaboration pia ilienda kwa : Jay-Z & Alicia Keys - Empire State of Mind


Chriss brown alia stajini akiperfom nyimbo za michael jackson hasa alipokua akiimba wimbo unaoitwa MAN IN A MIRROR

get down with waka waka 9t

Lamar atoa ofa kwa wanadada!

Hapa nazungumza nikiwa kitaa cha Kariakoo...kunako studio za Fish Crab...za bwana mdogo Lamar..ambaye anashikilia mkononi
tuzo ya kili ya mtayarishaji bora wa muziki wa mwaka.




ANASEMAJE MCHIZI HUYU

Ni kwamba mchizi anatoa offer bure ya kurekodi kwa underground wa kike popote pale walipo ndani ya bongo..ambao wanajihisi ama wanajiamini kuwa wana uwezo wa kurap au kuimba r&b,pop na mengineyo..na ambaye hayuko chini ya Record label yoyoye...kupeleka demo kwenye studio zake zilizopo eneo ya Jangwani karibu na klabu la Yanga ili ihakikiwe..na kama huna uwezo wa kutengeneza demo basi fika kwenye studio hizo na utapewa maelekezo ya kushiba uli ufanikishe azma yako! ewe mwanadada...time ndio hii..usipoteze muda.

Show za MBDOGGY zalalamikiwa Nchini UK

Msani MB-DOGG yupo nchini uingereza kwa ajili ya kupiga show kali nchini humo, But baadhi ya wadau wamelalamika na kutatizwa na MBDOGGY kutumia mtindo wa playback toka kwenye concert ambao Doggy katupia pale mji wa milton keynes ..

                                                                      MB DOGGY





PROMOTER WAPI LIVE BAND..NA NI KWANINI PLAYBACK ?????
Hapa sijajua kwamba msala nimtupie nani !!!!..tuanzie kwa huyu mletaji msani .promoter unamleta msani toka afrika alafu anaimba juu ya cd(playback) hapo lengo hasa la kumleta huyo msanii kwa wale mashabiki wake ni lipi...? kama anaimba na cd..mie nilikuwa nafikiria kuwa ma promoter jaribuni kuwa sistizia wasani ambao mna wapeni mashavu ya kwenda nje kutangaza sanaa yao..waiimbe kupitia live band sio mambo ya play back cd..hapo tutakuwa tunainua na kukuza vipaji na vile vile kunenepesha mifuko ya wasani hao..coz ..naona wasani wanao imba live music mashabiki wao wana furahi na vile vile kuwaleta wasani kama wale ni gharama coz wanatoa burudani halisi sio cd play back..lakini mkaka DOGGY hongera but step up the Game to live band music kaka ..hicho ndio kitu ambacho dunia inataka kutokwa kwa wasani halisi sio wababaishaji..

                                                  MB DOGGY PANDE ZA UK


FUNS WA MB DOGGY

MB DOGGY

Thursday, July 1, 2010

Mixtape ya Antivirus inatetea muziki wa bongo flava? Sugu Azungumzia kukamatwa kwake:

Nyimbo ya I Wanna Kill Ru.., unaopatikana kwenye mixtape hiyo umepelekea Sugu kuitwa na kuhojiwa na polisi. Pamoja na mistari ya nyimbo hiyo kuwa mikali kidogo, lakini je, ni kweli kuwa Sugu anataka kuua au ni utundu tu wa mashairi?

Mixtape hii imeibua hoja kadhaa, moja ikiwa ya uhusiano kati ya redio na wasanii, pamoja na nafasi ya redio katika kukuza sanaa nahata nafasi ya redio kuuwa sanaa. Neno bongo flava lilizaliwa redioni, na redioni huko huko ndipo bongo flava ilipolelewa na kukuwa mpaka hapa ilipofikia. Lakini je, redio zimefanya kazi ya kutosha kukuza ubunifu katika sanaa hii ya bongo flava? Kwani, swala la ma-Dj kuwa mameneja wa wasanii linapigiwa kelele kila siku, kwani ma-dj hao mamaeneja wanashukiwa kuwapendelea wasanii wao. Kama hii ni kweli, upendeleo huo ni ufa, tena ni ufa unaoweza kuhatarisha maendeleo ya sanaa hii inayoajiri vijana wengi.

Pamoja na yote, mashairi ya Sugu na wenzake katika mixtape hii yanaweza kuangaliwa katika pande mbili. Pande ya kwanza, ni kuwamashairi yao yanachochea chuki na hata kuleta fujo. Pande ya pili, ni kuwa mashairi yao yanaongea ukweli mtupu, na lugha kali waliyotumia ni kutokana na kuchoshwa na unyonyaji katika sanaa ya bongo flava. Inawezekana pia Sugu ameamua kujitoa muhanga na kutuonesha roho ya udhubutu, kwani Watanzania tuna sifa ya kukubali yaishe. Sasa basi, kama mashairi ya mixtape hii yataleta fujo, Sugu na wenzake watakuwa na kesi ya kujibu. Lakini kama tunakubaliana kuwa mabadiliko “changes” huja mara nyingi kutokana na mapambano ya aina fulani, basi Sugu ndio anatuonesha njia, kama Bob Marley alivyoimba Get Up Stand Up.

Swali, je Mixtape ya Antivirus inatetea muziki wa bongo flava dhidi ya wachache wanaouyumbisha au inataka kuchochea fujo zinazotokana na chuki kibinafsi? Sasa soma tamko rasmi alilotoa Sugu kwa vyombo vya habari juu ya kasheshe zilizomkumba siku mbili hizi tangia Mixtape ifike mtaani.
**********************************************************************************
Barua Ya sugu
napenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha wananchi wenzangu wa Mbeya Mjini, wapenzi wa muziki wangu, wanachama wenzangu wa CHADEMA na watanzania kwa ujumla tarehe 28 Juni 2010 nilikamatwa na polisi kwa kile walichonieleza kuwa kuna malalamiko dhidi yangu kuwa nimemtishia kwa maneno kumuua Ruge Mutahaba kupitia wimbo uitwao “Wanna Kill” uliopo kwenye album iitwayo “Anti Virus”.

Walinikamata saa 5 asubuhi nikiwa naingia ukumbi wa Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) kwa ajili ya kutoa Mada kuhusu “Tathmini ya Muziki wa Kizazi Kipya na Hatma yake nchini” na kunihoji kwa takrabani masaa matano mpaka saa 10 jioni.

Wameniachia kwa kile walichonieleza kuwa ‘dhamana ya kujidhamini mwenyewe’ na kunitaka niripoti kwao siku ya jumatano tarehe 30 Juni saa 5 asubuhi siku ambayo nilipanga kwenye ratiba zangu kurejea nyumbani Mbeya Mjini kwa ajili ya kuchukua fomu ya kugombea ubunge kabla ya tarehe ya mwisho ya utoaji na upokeaji fomu ndani ya CHADEMA.

Katika mahojiano nao yaliyofanyika Makao Makuu ya Upelelezi Wizara ya Mambo ya Ndani; maofisa usalama (CID) walionihoji walirejea mstari mmoja katika kiitikio cha wimbo husika wenye maneno “I Wanna Kill Right Now” na kusema kwamba mlalamikaji ameutafsiri mstari huo kuwa ni tishio la kutaka kumuua.


Napenda kuwajulisha mashabiki wangu na watanzania wenzangu kwamba nimelieza wazi jeshi la polisi kwamba hakuna wimbo wala maneno niliyowahi kutamka kwa lengo la kukusudia kumuua binadamu yoyote. Niliwaeleza jeshi la polisi kwamba sanaa ya muziki inalugha zake zake za kifasihi.

Maadhui ya wimbo mzima yamejikita katika harakati zangu za siku zote za kupambana na wanyonyaji dhidi ya maslahi ya wasanii Tanzania na wimbo huo una maudhui ya kutaka “Kuondoa ama kuiua dhamira ya mbovu na nia zao ovu”.

Ni vyema mashabaki wangu, wanachama wenzangu na watanzania kwa ujumla wakarejea katika Kamusi mbalimbali za kimataifa ambapoo neno KILL linamaana zaidi ya 10 zikibeba pia maana ya KUKOMESHA, KUONDOA nk.

Katika wimbo huo nimeghani kwa kutumia fasihi mambo ya ukweli yanayotokea katika sekta ya sanaa na wala hauna dhamira yoyote wala maudhui ya kufanya kosa lolote la jinai; hivyo kama kuna mtu ameguswa na ukweli uliomo katika wimbo huo na hakubaliani nao basi aupinge kwa hoja ama akafungue madai badala ya kukimbilia kutaka kuliingiza jeshi la polisi kwenye masuala ya sanaa.

Aidha nimeshangazwa na hatua ya jalada hilo la polisi kufunguliwa ndani ya Makao Makuu ya Jeshi la Polisi Wizara ya Mambo ya Ndani yaliyopo Wilaya ya Ilala wakati mimi na mlalamikaji wote ni wakazi wa Wilaya ya Kinondoni.

Baada ya maelezo niliyoyatoa ni matumaini yangu kuwa jeshi la Polisi ambalo lina kazi muhimu zaidi ya kukabiliana na ujambazi na vitendo vingine vya uhalifu ambavyo vinazidi kuongezeka katika Mkoa wa Dar es salaam ambapo Makao Makuu ya Jeshi la Polisi yapo litaelekeza nguvu zake katika kukabiliana na vitendo hivyo vya makosa ya Jinai badala ya kupoteza muda wake kushughulikia masuala ya kifasihi ambayo yana sura ya madai yasiyo na uzito wowote.

Fiesta 2010 kuanzia Mkoani Morogoro


                                                                       MARLAW

Tamasha la Fiesta 2010 linakaribia kuanza,na kama ujuavyo tamasha hilo husheheni mambo kibao kwa wapenzi/washabiki wao.safari hii kwa mara ya kwanza tena linagonga hodi ndani ya mji kasoro bahari,Morogoro.Wakazi wa Morogoro Fiesta hiyo 2010 inawajia mkoani mwenu ikiwa na kauli mbiu yake JIPANGUSE Rrrrrrrhhhhhhaaaaa..! Huku Mdhamini mkuu wa tamasha hio ambalo hufanyika mara moja kwa mwaka ni kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Ltd.


                                                              MWANA FA & AY

Orodha ya wasaniii utakao Jipanguse nao ndio kama hao hapo juu,si hao tu na kuna wegineo kadhaa wa kadhaa akiwemo Mwana Fa,Amini na Linah kutoka THT.Kutakuwepo na michezo mbalimbali,Fiesta Jipanguse rrrhhhhhaaaaa 2010 itafanyika ndani ya uwanja wa Jamhuri,July 7 kwa kiingilio cha sh 2000 kwa kila mmoja.Kama vile haitoshi July 9 tamasaha hilo litahamia mjini Arusha na kufanyika ndani ya Matongee .