BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Sunday, May 27, 2012

MWAKYEMBE AVAMIA TAZARA SAA 4 USIKU, Ni baada ya kupata taarifa kuwa treni ya mchana haijaondoka. Asema Uzembe wa watendaji ndio unasumbua abiria. Akaa Tazara mpaka Treni ilipoondoka Saa 6:00 usiku.


 Kiza cha wastani kimetanda kabla Mheshimiwa Dk. Harrison Mwakyembe hajawasili TAZARA.
 Mara Daktari anawasili kutaka kujua kunani?
 Akipewa maelezo kutoka kwa Meneja Mkuu wa Kanda Abdalla Shekimweli baada ya kutaka maelezo kwanini Treni haijaondoka hadi saa nne badala ya saa nane mchana.
 Akiwasikiliza kwa makini viongozi hao waliokua wakihaha kutoa majibu yakueleweka.
 Shekimweli akijitahidi kunyoosha maneno ili waziri amuelewe.
 Hapa waziri akaona bora waende wakalione hilo treni lenyewe!
 Dk. Mwakyembe akizungumza na abiria wa usafiri huo mara baada ya kupata maelezo kutoka kwa vingozi, nakuwaambia hakuna sababu yoyote ya maana iliyofanya wasiondoke ila ni uzembe tu. Amegundua kuna uwozo mkubwa kwenye menejimenti ya Shirika hilo ndio maana matatizo ya mara kwa mara yanatokea, huku abiria hao wakimshangilia. Mimi sikuwepo hapa nchini nimerudi jioni hii kutoka India lakini kuna abiria kama wawili wamenipigia kunieleza taarifa hizi ndiyo maana nimekuja kujua tatizo nini na nimegundua ni uzembe tu. Sababu kubwa iliyoelezwa ni kutokuwepo kwa mafuta lakini ni uzembe tu nitaushughulikia hivi karibuni.
" Kama shirika hili lingekua mali ya watanzania tu pekeyao basi sasa hivi ningetoa maamuzi usiku huu na nyie mngeona, lakini hatua ninayo ichuku sasa nimewaambia nataka treni iyondoke haraka mwisho iwe saa sita kuwepo abiria hapa! na siondoki hadi na hakikisha treni inaondoka," alisema Dk. mbele ya wananchi hao pichani.


 Abiria wa VIP nao alizungumza nao.

 Abiria wakichungulia kwa mbali wakati Dk. Mwakyembe alivyo akiwasulubu kwa maswali viongozi wa Shirika hilo.
 Mara abiria wakaanza kuitwa kupanda treni.
 Raia wa kigeni nao walikuwepo wakisota tangu saa nane mchana hadi mida hiyo ya saa sita usiku, huku Dk. Mwakyembe akiwaaga na wao kumpongeza.
 Tunakushukuru waziri bila wewe hapa tunge lala hapa! walisikika wakisema baadhi ya abiria.
 Baada ya abiria wote kuingia akapita kila behewa kuangalia kinachoendelea, hadi inaondoka.
 Hapa Dk. Mwakyembe anasubiri kichwa cha treni kije kuunganishwa ili liondoke. Baada ya kupata maelezo kuwa kinawekwa mafuta maeneo ya Yombo.
 Hapa zikionekana taa za kichwa hicho zikiwasili kwa mbaaali.
 Na sasa kimewasili rasmi kichwa.
 Kinaunganishwa taratiibu na treni.

Hatimae safari ikaanza na furaha ikitawala.

0 comments: