BLOGGER TEMPLATES AND TWITTER BACKGROUNDS »

www.thazealottz.blogspot.com

Promo

Saturday, September 4, 2010

LEO KATIKA JUKWAA LA FILAMU www.filamutanzania.blogspot.com



INI EDO, TONTO DIKE WAPATA SKENDO YA KUSAGANA.


Tonto Dike


Tangu Nollywood diva, Ini Edo aingie rasmi katika ndoa na, Philip Ehiagwina, mfanya biashara maarufu anaye fanyia shughuli zake marekani, amekuwa akipatwa na uvumi kuwa ana mahusiano na wanawake wenzake, kutokana na taarifa tofauti tofauti zinazovuma chini chini nchini Nigeria.
Kwamba katika ndoa yake na Philip kuna migongano na inasemekana kuwa amekuwa na wakati mgumu katika ndoa yake hiyo. Kuna habari zinazo vuma chini chini hivi sasa kuwa ana mahusiano na mwanamke mwenzake tabia inayotambulika kama ‘lesbianism’.



Ini Edo

Skendo hiyo ambayo inamuhusu yeye na Mwigizaji mwingine kutoka Nollywood, Tonto Dike na Ini Edo ambao inasemekana kuwa wote walionekana wamelewa hivi karibuni kwenye location na walionekana wakifanya vitendo vilivyo washtua watu. Kwa mujibu wa mtoa habari amesema kuwa,Ini Edo and Tonto, wameonekana wakiwa usiku mmoja wakiwa pamoja na wameonekana wakifatana kama mapacha katika sehemu mbalimbali za starehe kama Alpha Beach, Lekki area huko Lagos.

Tonto Dike anaishi maeneo Abraham Adesanya huko Ajah area Lagos.Na kwa mujibu wa habari kutoka katika mtandao wa www.nigeriafilms.com ulifanya utafiti na kuona hali ya ulevi na utupu umeingilia maisha ya wanadada hao.





MCHUMBA WA MERCY JONHSON AMUONYA NYOTA HUYO WA NOLLYWOOD, KUWA OFFLINE KWENYE FACEBOOK



MERCY JONHSON


Hii inaweza isiwe habari nzuri kwa shabiki wa mwanadada huyu, Mercy Johnson ambaye ni mtumiaji wa mtandao maarufu wa kijamii ambao hutumiwa kuwasiliana na kuchat wa Face book. Habari ni kuwa, mercy, ameonywa na mpenzi wake, Prince Odi kutotumia profile yake yaani kuwa offline mpaka pale watakapo oana. Kwa mashabiki wote, unataarifiwa kuwa muigizaji huyo, Mercy mpaka hivi sasa hajatumia facebook kwa takribani muda wa mwaka mmoja sasa. Sababu ikiwa mpenzi wake huyo, Prince Odinosen kamuonya kutoitumia facebook kama kweli anatarajia kufunga nae ndoa.

Kama ni mmoja wa watu uliyekuwa unapenda kuchati na Mercy Johnson kwenye facebook, ufahamu kabisa kuwa profile picture ni yaMercy lakini maneno yaliyomo yanaandikwa na mchumba wake Prince Odinosen.

0 comments: